Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa Mwaka wa Fedha 2025/2026

Hon. Mwantumu Mzamili Zodo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa Mwaka wa Fedha 2025/2026

MHE. MWANTUMU M. ZODO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nichukue fursa hii kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kunijalia afya njema. Pia nimpongeze Mheshimiwa Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa uchapakazi wake na jitihada za kuhakikisha anaendelea kutangaza na jitihada za kukuza utalii kwenye nchi yetu. Niendelee kumpongeza Mheshimiwa Waziri, Naibu Waziri na watendaji wote wa Wizara kwa uchapakazi wao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niishauri Wizara kwamba kwa kuwa Mheshimiwa Rais amefanya jitihada kubwa kuhakikisha utalii wa nchi yetu unakuwa hivyo Wizara nayo ifanye jitihada kwa kushirikiana na Wizara ya Miundombinu kuhakikisha barabara zote zinazoingia kwenye mbuga zetu zinapitika mwaka mzima. Kwa mfano, barabara inayotoka Mandela kuingia kwenye mbuga yetu ya Saadani wakati wa mvua haipitiki kabisa. Hivyo Wizara iendelee kufanya jitihada.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia changamoto ya tembo kuendelea kuvamia makazi ya wananchi bado ni kubwa sana. Kwa mfano kwa Jimbo la Mkinga katika maeneo ya Mwanyumba, Mavovo mpaka Mwakijembe changamoto bado ni kubwa sana. Hivyo niiombe Wizara kuendelea kuchukua hatua zaidi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaunga mkono hoja.