Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya kwa Mwaka wa Fedha 2025/2026

Hon. Joseph Michael Mkundi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukerewe

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya kwa Mwaka wa Fedha 2025/2026

MHE. JOSEPH M. MKUNDI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya wananchi wa Ukerewe nitoe shukrani kwa kuanza kwa ujenzi wa hospitali ya rufaa ngazi ya mkoa jimboni Ukerewe, kukamilika kwa hospitali hiyo itakuwa ni mkombozi wa maisha ya wananchi wengi. Niombe yafuatayo:-

(i) Majengo ya awali yaliyokuwa yanajengwa na SUMA JKT yaliyopo eneo la hospitali ya wilaya yakamilishwe haraka na kukabidhiwa halmashauri ili yapunguze shida ya miundombinu katika hospitali ya wilaya.

(ii) Ifanyike tathmini ya majengo yanayotumika kwa sasa kama ofisi za halmashauri na kama yatakidhi basi kianzishwe chuo cha uuguzi na uganga kwa sababu pale tuna jengo jipya la halmashauri, litakapokamilika basi majengo haya hayatakuwa na kazi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la upatikanaji wa huduma za afya kwa makundi ya wajawazito na watoto bure kama ilivyo sera bado lina changamoto nyingi sana, naomba kushauri Wizara iwe na kitengo maalum cha kufuatilia utekelezaji wa sera hii ili changamoto zinazojitokeza kwenye eneo hili ziwe zinapatiwa ufumbuzi na kuondoa malalamiko mengi kwenye jamii na kuepusha vifo kwa makundi haya.