Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa Mwaka wa Fedha 2025/2026

Hon. Dorothy George Kilave

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Temeke

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa Mwaka wa Fedha 2025/2026

MHE. DOROTHY G. KILAVE: Mheshimiwa Spika, ninamshukuru Mungu kwa uzima na afya kuimarika na kuendelea kutimiza wajibu wa kazi ya Kibunge.

Mheshimiwa Spika, nimpongeze sana Spika na wasaidizi wake wote kwa kuendesha Bunge kwa ukamilifu na ushirikiano. Pia nimpongeze Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kazi kubwa na nzuri kwa kuendelea kuijenga na kuilinda Jumuiya yetu kwa amani na upendo hali ambayo inatufanya Watanzania kujidai kwani amekuwa mama mnyenyekevu na msikivu.

Mheshimiwa Spika, niwapongeze Wizara hii ya Mambo ya Nje kuendeleza sera ya kujenga nchi yetu kwa kuendeleza mahusiano yetu na nchi za umoja huu. Niwapongeze mabalozi wetu kwa kufanya kazi zao za kibalozi kwa uaminifu na wamejitahidi kuchangamkia fursa hasa za kiuchumi, lakini niombe elimu itolewe kwa Watanzania ili fursa hizi ziweze kuchangamkiwa na wananchi kwa ujumla.

Mheshimiwa Spika, niendelee kumpongeza Rais wetu kwa kuendelea kukamilisha bajeti inayoombwa na Wizara hii kwani tumekuwa mfano bora kwa kulipa michango yetu katika Bunge la Umoja wa Afrika Mashariki

Mheshimiwa Spika, ninaomba kuunga mkono hoja.