Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Special Address by His Excellency Hon. William Samoei Ruto, PhD, C.G.H., President of the Republic of Kenya and Commander-In-Chief of the Defence Forces, to the Parliament of the United Republic of Tanzania

Hon. Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Special Address by His Excellency Hon. William Samoei Ruto, PhD, C.G.H., President of the Republic of Kenya and Commander-In-Chief of the Defence Forces, to the Parliament of the United Republic of Tanzania

WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, moyo usiyokuwa na shukurani hukausha yaliyo mema yote. (Makofi)

Kwa dhati ya moyo, umenipa nafasi hii kutoa shukrani kwa niaba ya wananchi wa Mkoa wa Tanga. Nimshukuru sana Rais, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa moyo wake na upendo wake wa kumkaribisha Rais wa Jamhuri ya Kenya, Dkt. William Samoei Ruto. Amezungumza mara nyingi sisi kwa wasaidizi wake kwamba Dkt. William Samoei Ruto ni kaka yake, na sisi kama wasaidizi wake, ametusisitiza mara kwa mara kufanya kazi kwa umoja na mshikamano. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ninataka nikuhakikishie Mheshimiwa Rais Dkt. William Samoei Ruto, mimi ni Waziri wa Maji ambaye nimepewa dhamana. Tunafanya kazi kwa ukaribu na Mheshimiwa Engineer Eric Mugaa, ambaye ni Waziri wako wa Maji na Umwagiliaji wa Jamhuri ya Kenya. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, dunia ya sasa inataka viongozi watakaoleta matokeo, na Baba wa Taifa aliwahi kusema uongozi siyo cheo, uongozi ni matokeo. Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan na Mheshimiwa Dkt. William Ruto, hawa ni viongozi wetu wa matokeo. Tuwapigie makofi mengi sana. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, Imam Shafii aliwahi kusema, nyoyo za binadamu zinaongeza mapenzi makubwa hasa kwa viongozi ambao wanatenda mambo yaliyo mema kwa watu wao. Kwa haya ambayo amezungumza Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Kenya pamoja na Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, hakika wataendelea kukumbukwa na kukumbukwa na kubaki katika historia kwa matendo mema ambayo wanawatendea hasa Watanzania pamoja na Jamhuri ya Kenya. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, mimi nimetokea Tanga, Mji wa Tanga tumekuwa tukitangatanga hasa katika maendeleo, lakini leo umezungumza hapa hakuna suala la ubinafsi katika maendeleo. Umesema refinery ikajengwe Tanga. Mungu atakubariki sana. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ninataka nikuhakikishie, tukiwa kama viongozi wa Mkoa wa Tanga, tumeupokea mradi huu wa kimkakati kwa umoja na mshikamano na wala hatutotangatanga. Tutaleta ushirikiano, tuna Mkuu wa Mkoa mzuri na tuna viongozi wazuri. Pamoja na Mheshimiwa Rais wetu na maelekezo ambayo atakayoyatoa, tutahakikisha mradi huu unakamilika kwa wakati na manufaa yanakuwa makubwa kwa Watanzania na Wakenya, pamoja na nchi hizi za Maziwa Makuu na wenzetu wa Uganda. (Makofi)

Mheshimiwa Rais, mimi sina maneno mengi sana ya kusema, ila kikubwa ukipata viongozi ambao wanawazia mema Watanzania pamoja na Wakenya, ni jambo kubwa. Mungu awabariki sana na Mungu atawalipa katika safari zenu. Ahsante sana Mheshimiwa Rais. (Makofi)