Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2026/2027

Hon. Juma Ramadhani Mustafa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Igalula

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2026/2027

MHE. JUMA M. KAWAMBA: Mheshimiwa Spika, kwanza kabisa ninaanza kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu ambaye amejaalia asubuhi hii tumekutana hapa ukumbini Bungeni, lakini Mwenyezi Mungu huyo huyo ambae amejaalia amani na utulivu ndani ya Taifa letu limeendelea kuimarika.

Mheshimiwa Spika, ninapenda kumpongeza Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan na Amiri Jeshi Mkuu wa Taifa hili kwa juhudi zake ameendelea kuhakikisha Tanzania yetu amani na utulivu imeendelea kuimarika. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ninapenda kumpongeza Waziri wa Wizara hii na viongozi wote wa vyombo vya ulinzi na usalama ambao wanahakikisha mipaka yetu ya nchi imeendelea kuwa na amani na amani na utulivu wa nchi yetu umeendelea kuimarika.

Mheshimiwa Spika, sisi sote tunakubaliana hapa hakuna maendeleo bila amani na hakuna amani bila ya kuwa na jeshi imara. Jeshi letu limekuwa ni mfano wa kuigwa Afrika Mashariki na Kusini mwa Jangwa la Sahara kutokana na uwekezaji wa muda mrefu ambao umeendelea kufanywa ndani ya jeshi letu. Hii inatuonesha nini sisi kama Waheshimiwa Wabunge, inabidi tuendelee kulipa ushirikiano jeshi letu ili liendelee kukabiliana na changamoto za ulinzi na usalama za kisasa. Kwani changamoto za ulinzi na usalama za kisasa ni ugaidi, uhalifu wa kimitandao, uuzaji wa haramu wa binadamu, lakini hii inatuonesha nini; sisi kama Wabunge inabidi tuendelee kulipa support jeshi letu kwa kulisemea na kuishauri Serikali, ihakikishe bajeti tutakayoipitisha hapa, fedha hizi zinakuja kwa wakati, kusudi jeshi letu liendelee kufanya kazi kwa weledi.

Mheshimiwa Spika, pamoja na mafanikio haya, lakini bado kuna changamoto mbalimbali ambazo tunatakiwa tuziangalie ndani ya jeshi letu. Sisi kama Waheshimiwa Wabunge inabidi tuendelee kuiomba Serikali, iendelee kuboresha makazi ya askari wetu, maeneo ya kufanyia kazi, maeneo ya maisha yao maaskari wetu, lakini matibabu ya askari wetu pamoja na kununua dhana za kisasa za kijeshi. Kwa sababu tunafahamu bila kuiomba Serikali iongeze bajeti na bajeti itakayopangwa iletwe kwa wakati, isipoletwa wanajeshi wetu hawa hawawezi kufanya kazi kwa weledi.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, mimi ninaiomba Serikali bajeti hii ambayo tutaipitisha hapa siku ya leo Serikali ijitahidi bajeti yote ije kwa ajili ya kuweza kuimarisha weledi na ufanisi wa jeshi letu. Kuna Jeshi la Kujenga Taifa, jeshi hili ni jeshi ambalo linafundisha uzalendo, linafundisha nidhamu, lakini pia linawawezesha vijana kuweza kuwafundisha mbinu mbalimbali za kuweza kujitegemea.

Mheshimiwa Spika, mimi ninaiomba Serikali iongezee bajeti Wizara hii, kusudi tuweze kuwa-accommodate vijana wengi waweze kujiunga na jeshi hili. Ikiwa ni pamoja na kurekebisha makambi, kuweza kuongeza makambi yawe na uwezo mkubwa wa kuweza kuchukua vijana wengi na mimi vijana wangu wa Jimbo la Igalula wawe pamoja ambao watakaochukuliwa kwa wingi na kuweza kujiunga na Jeshi la Kujenga Taifa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, Jeshi hili la JKT tukilitumia vizuri linaweza likatusaidia kupunguza upungufu wa ajira kwa vijana...

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

SPIKA: Mheshimiwa Juma, muda wako umekwisha, ahsante.

MHE. JUMA M. KAWAMBA: Mheshimiwa Spika, ninaunga hoja kwa 100%, ahsante ninashukuru sana.