Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maji kwa Mwaka wa Fedha 2026/2027

Hon. Mabula Johnson Magangila

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Msalala

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maji kwa Mwaka wa Fedha 2026/2027

MHE. MABULA J. MAGANGILA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwanafasihii. Kwanza kabisa, ninapenda kumshukuru sana Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mawaziri wa Wizara ya Maji kwa miradi ambayo imetekelezwa katika Jimbo la Msalala, yenye thamani ya shilingi bilioni 32.5.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kweli wananchi wa Msalala wanampongeza sana Mheshimiwa Waziri kwa fedha hizi nyingi ambazo ametuletea jimboni kwetu. Mheshimiwa Waziri amekuja na Mheshimiwa Rais wakati wa kampeni, tukawaambia tunayo miradi yetu ambayo bado haijakamilika. Mradi wa Nduku, Busangi, ambao unatakiwa utoke Nduku, Busangi, ufike Ntobo, makao makuu ya halmashauri. Tunaomba mradi huu uweze kukamilika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunao Mradi wa Mangwi, Ilogi, ambao unatakiwa utoke Mangwi, Ilogi, ufike Lunguya. Wananchi wa Lunguya wanausubiria sana mradi huu uweze kukamilika. Tunao mradi wa Mwamboku, Magongwa, ambao haujawahi hata kuanza, lakini wananchi wanausubiria kwa hamu sana, ili uweze kutatua kero ya maji katika Kata ya Kashishi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunao Mradi wa Vijiji 21, ambao huu unakwenda kugusa kata tisa. Kata tano ni ambazo zina vyanzo vya maji ya visima virefu, ambapo tayari visima virefu vipo. Kwa hiyo, ni ukamilishaji tu wa usambazaji wa maji katika visima hivyo. Unazungumzia Kata ya Ikinda, Kata ya Shilela, Segese, Mega na Chela.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunao mradi ambao, pamoja na kimya cha Mheshimiwa Waziri cha kukamilisha mradi ule ambao ulianza, sisi katika Jimbo la Msalala bomba la Ziwa Victoria limepita kwenye jimbo letu. Tunavyo vijiji tisa ambavyo vinapitiwa na bomba la Ziwa Victoria, ambapo mradi huu unagusa kata nne; Kata ya Mwalugulu katika Kijiji cha Sungamile, Kata ya Mwakata, Kata ya Isakajano, Vijiji vya Matinje na pia, unagusa Mradi ambao unatakiwa ukamilike wa vijiji viwili ambavyo viko kwenye Kata ya Isakajana, ambavyo ni Jana yenyewe pamoja na Butondolo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Jimbo la Msalala, Serikali ikikamilisha Mradi huu wa Vijiji 21 unakwenda kuwa na vijiji 75 kati ya vijiji 92 vya Jimbo la Msalala. Kwa kweli, atakuwa ametusaidia sana katika jitihada za kumtua ndoo mama kichwani. Miradi yetu hii mingi ni ya kufikisha maji kijijini. Gharama za kuvuta maji kufikisha majumbani bado ni gharama kubwa sana. CBWSOs zetu tayari zinafanya vizuri sana kwa sasa hivi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sisi baada ya kutufikishia maji haya kwa kiwango hiki, kuanzia mwezi wa Saba mpaka leo hii, kaya 428 zimeshaunganishwa maji, lakini bado gharama ni kubwa sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tuombe CBWSOs zetu ziendelee kutekeleza miradi midogo midogo ya kusogeza maji kwa wananchi, ili gharama ya kuvuta maji kutoka kwenye bomba kufikisha kwenye kaya za wananchi wetu ipungue na hiyo ndiyo maana halisi ya kumtua ndoo mama kichwani. Badala ya kwenda kuchota maji kwenye DP na kuleta nyumbani, tunataka wananchi wetu wachote maji majumbabi mwao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunao Mradi wa gridi ya Maji ambao tunasema, tutatoa maji Ziwa Victoria, lakini tunayo mikoa ambayo hata ukichimba maji chini unakutana na chumvi. Upi mpango wa Wizara wa kuvuna maji ya mvua ya kutosha?

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo hii tunao Mradi wa Lita za Ujazo Milioni Nane ambao ni wa Bwawa la Maji ya Mvua ulioachwa na Buzwagi, pale Kahama. Tunapeleka maji yale kwenye tenki letu la maji, pale shule.

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

MWENYEKITI: Ahsante.

MHE. MABULA J. MAGANGILA: Mheshimiwa Mwenyekiti, asante sana na ninaomba kuunga mkono hoja.