Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Contributions
nil
Answers
nil
Commettees
1
Ministries
nil
MHE. DKT. NEEMA P. MAJULE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kunipa nafasi hii ya kuchangia jioni. Nianze kwa kumshukuru Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wetu ambaye amefanya mambo makubwa sana. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninakumbuka kwa issue hii ya maji ni ajenda kabisa ya Rais wetu. Toka alipokuwa Makamu wa Rais, ajenda ya kila mwanamke ni ajenda ya Rais. Akiwa Makamu wa Rais amehakikisha alipambana na kupunguza vifo vya mwanamke na mtoto, akijipambanua kabisa kwamba yeye ni mwanamke. Pia amebeba ajenda hii ya maji kumtua ndoo mwanamke kichwani, lakini amebeba ajenda nyingine sasa hivi ya kumtua mwanamke kuni kichwani. Moja kwa moja ajenda yote ya mwanamke inakuwa ajenda ya Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan. Kongole nyingi sana ninampatia Rais wetu kwa kazi kubwa na kutuangalia sisi wanawake kwa jicho la tofauti. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninampongeza sana pia Mheshimiwa Jumaa Aweso. Nami ninasema ni Waziri wangu, akiwa Waziri hivi hivi aliniteua kuwa Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya DUWASA. Kwa hiyo, nimefanya naye kazi kwa karibu sana. Ninafahamu uwezo wake mkubwa wa kuchapa kazi. Ninampongeza sana Mheshimiwa Waziri, ninampongeza Naibu Waziri, ninampongeza Katibu Mkuu, sasa hivi mwanamke Mwajuma, anafanya kazi nzuri sana katika Wizara hii ya Maji. Tuna imani kubwa sisi wanawake wa Tanzania nzima ambao ndiyo tunatuliwa huu mzigo wa maji kichwani. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, hata hivyo niseme tu kwamba, Jiji letu la Dodoma linakuwa kwa kasi sana. Asilimia tano ya ukuaji wa miji hii mikubwa ambayo ndiyo inafanya hata kama production inaongezeka, hatuwezi kuona kwa kasi hivyo kutokana na ukuaji wa miji hii.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninamtia moyo mwanangu Mheshimiwa Jumaa Aweso. Aendelee kukazana tu kutafuta vyanzo mbalimbali vya maji. Dodoma water table ipo karibu sana. Hivyo wataalam waendelee kufanya geological survey waone kila maji yalipo yaweze kutoka kwa ajili ya manufaa ya wananchi wa Dodoma.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hata hivyo, niseme kwamba, Hayati Julius Kambarage Nyerere toka mwanzo alikuwa na nia ya kutoa maji kutoka Ziwa Victoria kuleta Dodoma. Alisema atachimba mfereji mrefu kutoka Ziwa Victoria hadi Dodoma. Azma hiyo amekuja kuitimiza Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, anataka kutimiza kwa vitendo. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Waziri wetu, maji ya Ziwa Victoria Dodoma tunayatarajia kwa matarajio yote na ambaye utatekeleza haya ni wewe. Kwa hiyo, sisi tunaona kwamba uandike historia kwenye uongozi wako wa Uwaziri; sasa maji haya yasiwepo kwenye makaratasi tena, yaje Dodoma. Kwa hiyo, kwenye kipindi hiki bajeti hii itakayopitishwa, anza moja kwa moja mkakati wa kuyaleta maji Dodoma. Nina imani kubwa ya kwamba utafanya hayo. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaomba nichangie mambo machache tu kwa ajili ya Wizara yetu ya Maji. Kwanza kabisa tufanye huo utafiti. Kitengo cha utafiti kiwe kikubwa kwa ajili ya kutafiti tunatafiti miamba yetu tunaangalia maji yalipo. Katika utafiti huu wataalam wetu waangalie pia mabadiliko ya tabianchi. Tunasema tunatoa maji kwenye maziwa yetu na mito yetu, lakini wafanye ulinganifu na mabadiliko ya tabianchi. Tusijekuwa tunachukua maji, tunapata maji, lakini tunaharibu pia mazingira yetu ambayo sisi wanadamu tunapaswa kuishi hapo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili, ambalo ushauri wangu uelekee kwenye maintenance, yaani kwa ajili ya kutengeneza miundombinu iliyochakaa. Upotevu wa maji bado upo 30% mpaka 35%, lakini tukijitahidi tukafika kile kiwango cha Kimataifa cha 25% kwa kufanya ukarabati wa miundombinu. Ninataka niseme pia kwamba, siyo ukarabati peke yake. Sisi hapa Dodoma tuna SAWA Group. Hawa ni vijana ambao kila siku wanaangalia maji yanavuja wapi na kutoa taarifa na tunafanya maintenance.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, ninampongeza sana Mkurugenzi wangu pia Aron Joseph, anafanya kazi nzuri ya kuzuia upotevu wa maji. Ninaiomba Wizara itenge emergence funds na pia itenge maintenance funds. Huku tunaongeza production huku tunafanya maintenance, lakini pia tunazuia upotevu wa maji. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, la tatu, ambalo ninapenda kushauri Mheshimiwa Waziri, ninaomba kushauri kuhusu prepaid meters; kwa kweli prepaid meters peke yake ndiyo suluhisho la jambo hili. Samahani ninamalizia. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, prepaid meters tungekuwa kama TANESCO, kwa hiyo hatutapata mambo ya ubambikizaji wa bills na vilevile the same time tutaweza ku-maximize profit ya mauzo yetu ya maji. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaomba kuunga mkono hoja, ahsante sana. (Makofi)