Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Sikonge
Contributions
nil
Answers
nil
Commettees
1
Ministries
nil
MHE. ENG. AMOSY W. MAGANGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote, ninakushukuru sana kwa kunipa nafasi hii. Kabla sijaanza mchango wangu ninaomba, kwanza nilete salamu za wananchi wa Mji wa Sikonge wenye kata mbili.
Mheshimiwa Mwenyekiti, wananchi hawa kupitia kwa Madiwani wao, Mheshimiwa Joyce Ng'amba wa Kata ya Mishen na Mheshimiwa Hamisi Saidi Kumba wa Kata ya Sikonge, wanaleta shukrani zao za dhati na za upendo kwa Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kwa kazi kubwa aliyoifanya ya kuwaondolea kero ya maji.
Mheshimiwa Mwenyekiti, wananchi hawa sasa wanapata maji ya uhakika kutoka Ziwa Victoria. Wanachokiomba sasa ni Mheshimiwa Rais aweze kufika kule Sikonge, ili yeye mwenyewe aweze kuuzindua huo mradi. Mwisho wa shukrani hizo kutoka kwa wananchi wa Sikonge, ninaomba sasa ili niweze kutoa mchango wangu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote, ninaanza kumpongeza Mheshimiwa Rais kwa kazi kubwa anayoifanya. Leo tunavyoongea wananchi wa Sikonge takribani 68% tayari wana miundombinu na vilevile wana maji. Kuna changamoto ndogondogo ambazo zipo kule, wakati mwingine maji hayatoki kama jinsi ambavyo wanavyotaka, lakini tunasema safari ni hatua. Ninaamini kuna siku wananchi wote wa Skonge watapata maji ya uhakika, saa 24 kwa siku saba.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninampongeza sana vilevile Mheshimiwa Waziri na Naibu Waziri. Ninakushukuru sana Mheshimiwa Waziri amefika kule Sikonge akashuhudia tone la kwanza la maji yaliyotoka Ziwa Victoria, ambayo ndiyo mwanzo wa Gridi ya Taifa. Ninampongeza sana Mheshimiwa Waziri na Watendaji wote wa Wizara ya Maji, ninawapongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, huu Mradi wa Maji kutoka Ziwa Victoria umepita, lakini ninamwambia Mheshimiwa Waziri kwamba, kuna kata takribani tisa ambazo ziko ndani ya kilometa 12. Nilipopita wakati ninamwombea kura Mheshimiwa Rais, pamoja na mimi mwenyewe na Madiwani, niliwaambia kwa uthabiti na kwa ujasiri kwamba, wasiwe na wasiwasi Mheshimiwa Mama Samia atawaletea maji kwa sababu, bomba linapita hapo katikati yao.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Kata hizo ni pamoja na: Pangale, Mpombwe, Igigwa, Kisanga, Tutuo, Mole, Mkolye, Chabutwa pamoja na Kata ya Ipole, hawa wananchi toka juzi wananipigia simu, tena wengine kwa machozi kabisa na nikawaambia machozi yenu ninayabeba na nitayafikisha kwa Mheshimiwa Aweso na ninaamini Waziri atakapokuwa ana-wind up atakuwa na jambo la kuwaambia wananchi hao.
Mheshimiwa Mwenyekiti, …
(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)
MHE. ENG. AMOSY W. MAGANGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante nimeshachangia kwa maandishi utayaona, basi ninaunga mkono hoja. (Makofi)