Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions from Hon. Lucy Simirya Kombani (1 total)

MHE. LUCY D. S. KOMBANI: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Kwa kuwa hii migogoro imekuwa ya muda mrefu sana na inaleta madhara makubwa sana kwenye hizi jamii zetu na kwa upande mwingine tukiangalia tuna wataalam ambao wamesomea utatuzi wa migogoro; je, Serikali haioni haja sasa ya kuwatumia wataalam hawa katika kumaliza haya matatizo? (Makofi)
NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. JAFAR R. SEIF): Mheshimiwa Spika, ninaomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, itakumbukwa kwa kipindi cha mwaka 2023 hadi 2025 hakujaripotiwa migogoro yenye kuleta mapigano katika maeneo mengi nchini. Serikali inamuahidi Mheshimiwa Mbunge tutaendelea kuwatumia wataalam hawa ili kuweka hali hii ya usalama wa wakulima na wafugaji. Tunaendelea kuhamasisha zile kampeni (kwa mfano, Kampeni ya Tutunzane) ili kuona kabisa wakulima na wafugaji wanavyohitajiana na waweze kuishi katika maeneo kwa usalama na uzalishaji mali uendelee.