Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions from Hon. Janeth Peter Pinda (1 total)

MHE. JANETH P. PINDA: Mheshimiwa Naibu Spika, ninakushukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali ya nyongeza. Swali la kwanza; kwa kuwa katika barabara hii ina vipande na Wakandarasi wa kutoka Vikonge – Luhafwe, lakini kutoka Luhafwe – Mishamo, wakandarasi hawapo site. Je, ni lini Serikali itatoa pesa kwa ajili ya ukamilishaji wa kipande hiki cha barabara?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili; Barabara hii kutoka Katavi – Uvinza na Serikali imeweka utaratibu au mpango wa kuunganisha barabara. Je, ni lini Serikali itakamilisha barabara hii ili kuondokana na adha ya usafiri kwa wananchi wa Mkoa wa Katavi pamoja na Kigoma? Ahsante.
NAIBU WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Naibu Spika, ninataka tu nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba kipande hiki cha Luhafwe – Mishamo ambacho kinajengwa na CHICO kulikuwa na changamoto kidogo, lakini tumeshaitatua na Mkandarasi anarudi site kuendelea na kazi.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu swali lake la pili la barabara ya kuunganisha Mkoa wa Katavi na Mkoa wa Kigoma pamoja na Mkoa wa Rukwa. Kutoka Kibaoni – Stalike, Mkandarasi alikuwa anasuasua tayari ameshalipwa malipo yake na yuko site anaendelea ili kuunga Kibaoni – Mlele – Stalike. Nimpe Mheshimiwa Mbunge habari njema kabisa kwamba, tunaenda kuunga Katavi na Kigoma kuanzia Mishamo – Uvinza, kandarasi itatangazwa muda siyo mrefu kukamilisha hizo kilomita zote 95. Muda siyo mrefu tunakwenda kutangaza hiyo tenda kila kitu kipo tayari. Kwa hiyo tutakuwa tumeunganisha kutoka Kibaoni – Uvinza – Mishamo – Mpanda hiyo ndiyo kazi ya Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan kuiunganisha mikoa. Ahsante.