Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Contributions by Hon. Saidi Salim Hamad (1 total)

Mpango Elekezi wa Maendeleo wa Muda Mrefu 2026/2027–2050/2051, Mapendekezo ya Mpango wa Nne wa Maendeleo wa Taifa wa Miaka Mitano 2026/2027–2030/2031 na Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa wa Mwaka 2026/2027; na Mapendekezo ya Mwongozo wa Maandalizi ya Mpango na Bajeti ya Serikali Katika Muda wa Kati ya 2026/2027 hadi 2028/2029.
MHE. SAIDI SALIM HAMAD: Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote sina budi kumshukuru Mwenyezi Mungu kuwa kunijaalia miongoni mwa watu ambao wako katika nyumba hii takatifu. Aidha, kwa vile ni mara yangu ya kwanza ninapenda kuchukua nafasi hii kukishukuru kwa dhati ya moyo wangu Chama changu Cha Mapinduzi kuanzia ngazi ya Jimbo, Wilaya, Mkoa; ngazi ya Ofisi Kuu Kisiwandui, pamoja na Kamati Kuu ya CCM Taifa, chini ya Mwenyekiti wake mahiri, Dkt. Samia Suluhu Hassan. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, aidha, ninachukua nafasi hii kumpongeza kwa dhati kabisa Dkt. Samia kwa ushindi wa kishindo alioupata tarehe 29 Oktoba, 2025. Baada ya shukrani hiyo, ninaomba nichangie hoja iliyopo Mezani kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa upande wangu nitajikita kwenye mambo makuu mawili. Mambo haya yataelekea kwenye implementation ya bajeti yetu hii ambayo iko mezani kwa Mwaka 2026/2027. Jambo la kwanza, ili tuweze kufanikiwa katika bajeti yetu hii wachangiaji tumechangia tufanye investment kubwa kwenye masuala mazima ya kilimo, biashara na madini. Kwa uono wangu, ninapenda niongeze sehemu nyingine ya investment kubwa ambayo tunapaswa kuwekeza, ni katika vijana wa Taifa hili. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mujibu wa sensa vijana ni more than 75%, lakini rika la watoto baada ya miaka miwili au mitatu nao wana-turn kutoka kwenye childhood wanakuja katika rika la vijana, so in general vijana wanachukua namba kubwa ya watu katika Taifa hili. Tukiweza kuwekeza katika sekta hizi zinazowahusu vijana tutaweza kuchangia pato la nchi hii na kuchangia katika bajeti yetu hii kwa kiwango kikubwa sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunaweza kuwekeza kwa vijana kupitia elimu, habari, teknolojia na michezo. Kupitia elimu vijana tunawasomesha masomo ya physics, biology, chemistry, history na masomo mengine mbalimbali, lakini kuna wimbi kubwa la vijana akili zao zimekita sana katika masuala ya michezo. Ninaishauri Serikali tuanze kuwekeza kupitia sports academies. Michezo sasa hivi ni biashara kubwa sana na tayari inachangia mapato makubwa katika mataifa ambayo yameendelea kwa kuajiri wachezaji wa mipira na michezo mbalimbali duniani na kuweza kupata mapato mbalimbali katika Taifa husika. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, iwapo tutaanzisha hizi sports academies kuanzia ngazi za watoto hadi vijana, vijana wetu wengi wataweza kujiajiri na kuajiriwa kupitia hii sekta ya michezo. Hata hivyo, tunapaswa kuwekeza kuanzia kwenye shina. It means tuajiri walimu professional, kwa ajili ya michezo, ambao wataweza kusomesha watoto kuanzia ngazi za nursery, primary, secondary na hata ngazi za vyuo vikuu kuwe kuna syllabus kabisa ya kusomesha haya masuala ya michezo, ili tupunguze wimbi kubwa la vijana ambao hawana ajira. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo ambalo litatuwezesha kupata fedha zaidi katika zoezi letu hili la bajeti ambalo tunakwenda nalo sasa hivi ni kupitia habari. Tumemwona Mheshimiwa Waziri Makonda, Mheshimiwa Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan ametenga shilingi bilioni mbili kuwawezesha content creators, hii ni ajira kubwa sana kwa vijana. Kama tutaweza kuwa-facilitate vizuri, Mama kaleta hizi shilingi bilioni mbili zikiweza kutumiwa very effectively basi zitakuza kipato cha vijana wetu kutoka hatua moja kwenda nyingine. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kupitia hili ninashauri kwa vile tuna benki mbalimbali hapa kwenye nchi yetu, tuna benki ya kilimo tumeianzisha. Kwa nini tusianzishe benki ya maendeleo ya vijana?

Mheshimiwa Mwenyekiti, ili hizi fedha ambazo zimetengwa, shilingi bilioni mbili, kupitia Wizara ya Habari, first ziwe deposited pale kwenye benki yetu, kwa ajili ya vijana. Tumesikia Mheshimiwa Rais kupitia Waziri wetu wa Vijana ambapo katuwekea Mheshimiwa Nanauka pale, katenga shilingi bilioni 200, kwa ajili ya kuwawezesha vijana. Kwa nini fedha hizi zisiwe first deposited kupitia benki yetu maalum ya vijana, ili vijana waweze kwenda kutumia fedha hizi katika sehemu zao maalum na wakitaka mikopo, wakitaka kuwa-facilitated kwenye mambo yao mbalimbali vijana hawa waweze kwenda kuchukua pale kwenye benki yetu hii?

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile kupitia maono ya Dkt. Samia Suluhu Hassan, ili tuweze kukuza uchumi wetu na kuweza kupata fedha ambazo zitasababisha bajeti yetu kukua siku hadi siku na uchumi wetu kupanda, kama ilivyo nchi yetu uchumi wake unakua kwa kasi zaidi na tunawekeza pesa nyingi kupitia sekta ya ujenzi, uchukuzi na miundombinu. Hapa Serikali kwa mwaka tuna-allocate billions of money ambazo zinaenda kujenga miradi mbalimbali katika Taifa letu, lakini katika fedha hizi ambazo zinaenda kuwekwa pale tunaenda kukuza uchumi wetu at the same time tuna-facilitate uchumi wa nchi nyingine. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunapo-compete kampuni za international na kampuni zetu local tunashindwa kushindana na kampuni zile zinazokuja kutoka nje ya nchi kwa sababu kuu tatu; kampuni zinazokuja kutoka nje ya nchi zinatushinda technical, financial na working experience. Zikija tukikaa nazo mezani, tuki-bid nazo pamoja, hizi kampuni za ujenzi na kujenga miundombinu mbalimbali zinashinda zile tenda. At the same time tunatumia fedha, billions of money ambazo Mheshimiwa Samia ana-allocate kupitia Wizara hizi kujenga miundombinu ya nchi yetu, lakini tunakwenda kuchochea uchumi wa nchi nyingine kwa sababu, zile kampuni zinapopata tenda ndani ya nchi yetu zina-take profit from these tenders and then wanaenda kujenga kwenye mataifa yao. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa hapa ninaishauri Serikali, ili tupate fedha hizi ziweze kukuza uchumi wetu, lakini vilevile iwe ni sababu ya ku-facilitate ukuaji wa maendeleo kwa jamii yetu. Tutengeneze mazingira rafiki kwa kampuni zetu za ndani ziweze ku-compete kuanzia internally mpaka externally. It means hapa, kama Serikali, tutatenga fedha tuzi-fund hizi kampuni. Kama tutakaweka Sheria fulani, let’s say imekuja kampuni kubwa kutoka China, imekuja kujenga flyover hapa, tukaweka Sheria kupitia kampuni hii ambayo imekuja, basi ifanye joint venture na kampuni yetu local.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tuweke Sheria kama hii, kazi total ni shilingi bilioni 200, lakini you must give sub-contract from a local company, ili kupitia sub-contract hii ambayo itapewa hii local company kuna mambo tutaweza kuya-gain. Tutaweza ku-gain experience from international company, lakini ile kampuni yetu ambayo ni local, instead ya kukaa bila kuipata ile kazi kubwa itakuwa nayo imepata kazi; itaweza kuajiri vijana mbalimbali na hawa Gen-Z ambao wako mtaani ambao wanamnyima usingizi Mama Samia, mama anapenda kuwaona vijana wake wamepata ajira. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ili apate usingizi mnono basi ni lazima tuwezeshe kampuni zetu za ndani, mama aweze kulala aone vijana wake wote wamepata ajira kupitia kampuni hizi za ujenzi ambazo zinakuja kufanya miradi mbalimbali. Tutapata experience na ile key personnel, wale technical staff ambao tuponao wakishirikiana na technical staff kutoka kampuni kubwa watajenga technics ambazo wanazitumia ku-complete hizo project kubwakubwa na mambo mengine mbalimbali. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaomba nimalizie kuchangia kwangu katika hoja hii kwa kusema maneno matakatifu kutoka katika Vitabu Vitakatifu. Ninaanza kunukuu kutoka Kitabu Kitakatifu; Ayubu 42:2 anasema; “Ninajua ya kuwa, wewe waweza kufanya mambo yote na ya kuwa makusudi yako hayawezi kuzuiliwa.” Kwenye Qurani kuna maandiko yanasema, “Qaddara Allahu wamaa shaa fa’ala.” Vilevile, kuna aya inasema; “Innama amruhu idha araada Shay’an an yaquula lahu kun faya kun.” (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninawaomba Watanzania wamwachie mama afanye kazi. Mama yupo kazini amesimamishwa kwa kadari ya Mwenyezi Mungu na hawezi kutetereka isipokuwa kwa kadari ya Mwenyezi Mungu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaunga mkono hoja. Ahsante sana. (Makofi)