Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions from Hon. Hija Hassan Hija (1 total)

MHE. HIJA HASSAN HIJA: Mheshimiwa Spika, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Waziri, ninaomba nimuulize swali moja la nyongeza. Mwezi Novemba, Mheshimiwa Waziri Mkuu alifanya ziara kwenye hospitali moja hapa Mjini Dodoma na wananchi, hususan wazazi, waliipongeza Serikali kwa huduma nzuri za matibabu na dawa, lakini walilalamikia ukosefu wa mabeseni na ndoo, kwa ajili ya wajawazito; Mheshimiwa Waziri Mkuu akaagiza jambo hili litatuliwe. Ninaomba kujua limefikia hatua gani?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. RAJAB S. JAFAR): Mheshimiwa Spika, ninaomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Hija Hassan Hija. Tunakumbuka ziara ya Mheshimiwa Waziri Mkuu kwenye kituo chetu, kile cha afya na akatoa maelekezo yale.

Mheshimiwa Spika, maelekezo ya Mheshimiwa Waziri Mkuu ndiyo maelekezo ya Serikali. Nami kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu, TAMISEMI, ninawaelekeza Waganga Wakuu wote wa Mikoa, Waganga wote, ma-DMO wa Halmashauri na ma-MOI wetu waendelee kutekeleza majukumu hayo, waendelee kutekeleza maelekezo ya Mheshimiwa Waziri Mkuu kwa maana kwamba, sasa mambo ya kuwatoza hivyo vifaa kama mabeseni na ndoo visiwe vikwazo kwa mama zetu wanapokwenda kujifungua katika hospitali zetu