Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions from Hon. Said Ibrahim Mzimba (1 total)

MHE. IBRAHIM S. MZIMBA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa majibu mazuri ya Mheshimiwa Waziri. Kwa kuwa vituo hivi vinahudumiwa na ndugu zetu wa polisi ambao wanafanya kazi kubwa sana ya kulinda nchi yetu. Je, Mheshimiwa Waziri, yupo tayari kuambatana nami kwenda Jimbo la Mtambile kujionea hali halisi ya makazi ya polisi wetu hawa?
NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, nishukuru kwa swali la nyongeza la Mheshimiwa Said Ibrahim; na ombi lake la kwenda Mtambile nimelipokea na nipo tayari kuambatana naye kwenda Mtambile.