Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions from Hon. Patali Shida Patali (1 total)

MHE. PATALI S. PATALI: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa fursa hii nami nipate kuuliza swali la nyongeza kutoka kwenye swali la msingi Na. 138. Je, ni lini Serikali itaupandisha hadhi Mji Mdogo wa Mbalizi kuwa Mamlaka ya Mji kamili, ikizingatiwa mji huu umekidhi vigezo vyote ikiwepo idadi ya watu, uwezo wa kujiendesha wenyewe? Pia mji huu umeomba kupandishwa hadhi muda mrefu sana?

Mheshimiwa Naibu Spika, ninaomba kwa niaba ya Wanambeya Vijijini nipate majibu ya Serikali. Ahsante sana. (Makofi)
NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. KWAGILWA R. NHAMANILO): Mheshimiwa Spika, ninawaelekeza uongozi wa Mkoa, husika wakamilishe michakato yote ambayo imeainishwa kisheria, ikiwa ni pamoja na kuanza mijadala kwenye ngazi ya Mitaa na Kata, Wilaya kwenye vikao vya RCC, vikao vya DCC. Watakapokamilisha wawasilishe TAMISEMI kama utaratibu unavyotaka, TAMISEMI tutatuma timu na tutafanya mapitio ya vigezo hivyo na kama vigezo vitakidhi, mamlaka itachukua hatua zinazofuata. (Makofi)