MHE. DKT. CHRISTINA C. MNZAVA aliuliza: -
Je, lini Serikali itajenga Zahanati Kata ya Nsalala Wilayani Shinyanga?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. JAFAR R. SEIF) alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaomba kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Christina Christopher Mnzava, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, TAMISEMI kama ifuatavyo: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mwaka wa fedha 2024/2025 Serikali imetoa shilingi milioni 44.45 kwa ajili ya ukamilishaji wa boma la zahanati katika Kata ya Nsalala. Aidha, Serikali katika mwaka wa fedha 2025/2026 imetenga shilingi milioni 22, kupitia mapato ya ndani ya Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga, kwa ajili ya ukamilishaji. Ujenzi wa zahanati ya Nsalala utakamilika na kuanza kutoa huduma kabla ya mwezi Juni, 2026.