Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions from Hon. Dr. Advocate Damas Daniel Ndumbaro (1 total)

MHE. DKT. DAMAS D. NDUMBARO: Mheshimiwa Naibu Spika, ninakushukuru sana kwa kunipa nafasi hii. Kata ya Seed Farm, Manispaa ya Songea, haina sekondari ya kata. Je, ni lini Serikali itajenga sekondari ya kata katika kata hiyo ya Seed Farm?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Mbunge wa Songea Mjini, kaka yangu Ndumbaro, amefuatilia mara kadhaa suala la ujenzi wa shule ya sekondari katika Kata ya Seed Farm, Manispaa ya Songea. Ninaomba nimhakikishie tu kwamba, tuko hatua za mwisho. Tulikubaliana na wataalamu wafanye tathmini ya vigezo na baada ya hapo tuhakikishe tunapeleka fedha, kwa ajili ya kuanza ujenzi.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, ninaomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba, tutahakikisha baada ya kupokea vigezo hivyo na kufanya tathmini, tutatoa kipaumbele kinachotakiwa kupitia mapato ya ndani ya Manispaa ya Songea na Serikali Kuu, ili tuweze kujenga shule hiyo ikiwa vigezo vitakuwa vimefikiwa.