MHE. JAPHET N. HASUNGA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa, Mji wa Vwawa ni moja ya miji ambayo iko kwenye hii Miradi ya TACTIC Awamu ya Tatu. Je, ni lini Serikali itaanza kutekeleza mradi huo katika Mji wa Vwawa? Ahsante sana.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. KWAGILWA R. NHAMANILO): Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli Mji wa Vwawa ni miongoni mwa miji 18 ambayo tunakwenda kutekeleza huu Mradi wa TACTIC. Kama nilivyojibu kwenye swali langu la msingi, tunakwenda kuanza utekelezaji wa mradi huu mara baada ya shughuli hizi za usanifu kukamilika. (Makofi)