MHE. CHRISTINA S. MNDEME: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi hii na mimi niulize swali la nyongeza. Katika Zahanati ya Imalakaseko iliyopo Kata ya Goweko, Halmashauri ya Wilaya ya Uyui, Mkoa wa Tabora, Serikali ilitoa shilingi milioni 80 kwa ajili ya ujenzi wa wodi ya mama na mtoto lakini wodi hiyo bado haijakamilika. Je, ni lini sasa Serikali itakamilisha ujenzi wa wodi hiyo ya mama na mtoto katika zahanati ya Imalakaseko, Kata ya Goweko, Halmashauri ya Wilaya ya Uyui? Ahsante. (Makofi)
NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. JAFAR R. SEIF): Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Mbunge amegusia hasa katika zahanati ya Imalakaseko, Halmashauri ya Uyui. Kwanza Serikali imeshatenga shilingi milioni 80 kama Mheshimiwa Mbunge alivyosema. Pia, ninamwelekeza Mkurugenzi kuendelea kutenga fedha za ndani Halmashauri ya Uyui ili kuweza kukamilisha ujenzi wa zahanati hii. (Makofi)