MHE. ENG. JOHNSTON J. MUTASINGWA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Ninapenda kuuliza swali la nyongeza kuhusu barabara zangu za Jimbo la Bukoba Mjini. Barabara ya kutoka Chemba kwenda Rugambwa, yenye urefu wa kilometa 1.4 na Barabara ya kutoka Kashai kwenda Mngeza, yenye urefu wa kilometa 7.41 zitaanza kujengwa lini kwa kiwango cha lami, kama ilivyoainishwa kwenye IIani ya Chama Cha Mapinduzi? Ahsante.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. KWAGILWA R. NHAMANILO): Mheshimiwa Spika, barabara hizi za Bukoba Mjini zitaanza kujengwa kwa kiwango cha lami, kama ambavyo imeainishwa kwenye Ilani ya Uchaguzi, mara tu baada ya Serikali kupata fedha na kutenga, kwa ajili ya shughuli hiyo.