Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions from Hon William Kafiti Kafiti (1 total)

MHE. KAFITI W. KAFITI: Mheshimiwa Spika, ninashukuru kwa nafasi hii ya kuuliza swali la nyongeza. Kutokana na majibu mazuri ya Mheshimiwa Waziri, bado sisi kama Mwanza na kama wakazi wa Jimbo la Ilemela, tunahitaji kujua huo upembuzi yakinifu utakamilika lini?

Mheshimiwa Spika, swali la pili, ukamilishwaji wa uwanja huu...
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Kafiti Mbunge wa Ilemela alikuwa anajaribu kukazia hoja ile ile ya uwanja wa ndege na kimsingi yeye pale kwake hoja kubwa ambayo anaizungumzia ni upande wa fidia au namna ya kuweza kuondoa wananchi wa pale. Serikali ina dhamira ya kuufanya Uwanja wa Ndege wa Mwanza kuwa wa kimataifa. Ili uweze kuwa na sifa hizo, lazima kama kuna wavamizi waondolewe. Kwa hiyo, nimwombe tu awe na subira, tutamilisha muda siyo mrefu tutaanza kufanya kazi.