MHE. HAIDARY H. SUMRY: Mheshimiwa Naibu Spika, ninakushukuru sana. Barabara ya Stalike – Mpanda mpaka Mpanda Ndogo imejengwa mwaka 2012, lakini bado wananchi wa maeneo hayo hawajalipwa fidia. Ninauliza ni lini wananchi hawa ukizingatia muda huo kuanzia 2012 watalipwa fidia yao?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Naibu Spika, ninaomba kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge, kama afuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kama alivyosema toka mwaka 2012, nitamwomba Mheshimiwa Mbunge tuweze kuonana naye ili kujua changamoto ni nini, kwa sababu 2012 ni muda mrefu. Nimuombe tu Mbunge baada ya hapa tuweze kuona ni wananchi wapi ambao hawajalipwa na wanastahili hayo malipo yake. Ahsante.