MHE. ASHA JUMA KOMBO aliuliza: -
Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga upya Kituo cha Polisi cha Mfenesini?
NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninamshukuru sana Mheshimiwa Asha na ninampongeza. Hivyo kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, ninapenda kujibu swali la Mheshimiwa Asha Juma Kombo, Mbunge wa Mfenesini, kama ifuatavyo: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali ina mpango wa kujenga kituo kipya cha Polisi Daraja āCā katika eneo la Mfenesini, ambacho kitagharimu kiasi cha fedha shilingi 165,228,990. Fedha hizo zinatarajiwa kutengwa kwenye bajeti ya Serikali ya mwaka wa fedha wa 2027/2028. Ninaomba kuwasilisha.