Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions from Hon. Suleiman Mohamed Rashid (1 total)

MHE. SULEIMAN MOHAMED RASHID: Mheshimiwa Spika, ahsante nimpongeze Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu mazuri lakini pamoja na majibu hayo nina swali la nyongeza. Serikali haioni haja kuandaa mwongozo wa dharura wa uboreshaji ambao utaweza kuzingatia kulipwa kwa posho ya kujikimu pamoja na posho maalum kwa walimu ambao wanasahihisha mitihani hiyo?
NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Spika, kwa ruhusa yako, ninaomba nijibu swali la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali imekuwa ikiboresha maslahi ya walimu wanaosahihisha mitihani kulingana na upatikanaji wa fedha ambapo pamoja na posho wanazolipwa Serikali pia hulipa malazi, chakula, matibabu wakati wote wa kazi. Hata hivyo, ushauri wa Mheshimiwa Mbunge tumeupokea. (Makofi)