Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions from Hon. Revocatus Chipando Clayton (1 total)

MHE. CLAYTON R. CHIPANDO: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili madogo ya nyongeza.

SPIKA: Mheshimiwa ni swali moja tu.

MHE. CLAYTON R. CHIPANDO: Mheshimiwa Spika, sawa. Ninaomba majibu kutoka kwa Serikali kuhusiana na Barabara ya Kasulu, barabara ambayo itakwenda kuwasaidia wananchi wa Kata za kama Machinjioni, Rubuga, Kagera pamoja na Kata ya Majengo. Barabara iliyopo sasa hivi inawalazimisha wananchi hawa wakitaka kwenda kwenye kata zao lazima wafike mjini halafu warudi nyuma. Ikijengwa Barabara hii ya Kasulu kuanzia pale Msimba kuelekea Ujiji itasaidia wananchi hawa wasiingie mjini wapate shortcut ya kwenda kwenye makazi yao. (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Spika, ninaomba kumjibu Mheshimiwa Mbunge Baba Levo, Mbunge wa Kigoma Mjini kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, tuna wakala mbili za barabara, TANROADS na TARURA. Mheshimiwa Mbunge, Barabara tunazozijenga sisi ni kuanzia Ujiji hadi Kigoma Mjini, Mwanga kwenda Mwandiga, pale kwenye Sanamu ya Sokwe kwenda Simbo na Mwandiga. Hizi barabara nyingine tutahakikisha kwamba tunawasiliana na wenzetu wa TARURA ili kuhakikisha hizo barabara zinajengwa na wananchi wasipate changamoto kama alivyozielezea Mheshimiwa Mbunge. Ahsante. (Makofi)