Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions from Hon. Kassim Hassan Haji (1 total)

MHE. KASSIM HASSAN HAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Ninamshukuru Naibu Waziri kwa kujibu majibu kwa ufasaha, lakini ninaomba niwape ushauri tu. Kwa kuwa treni hizi zinaondoka muda wa saa moja na nusu kupishana, kwa nini wasisogeze mbele hizi safari ikawa kama moja inaondoka saa tatu na nyingine iondoke saa saba mchana ili kuweka hawa watu wa katikati waweze kupata nafasi ya wao kusafiri?

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninawashauri sana Wizara waende wakaliangalie hilo, ahsante sana. (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nimepokea.