Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions from Hon. Moshi Selemani Kakoso (1 total)

MHE. MOSHI S. KAKOSO: Mheshimiwa Naibu Spika, Kituo cha Afya cha Karema, Kituo cha Afya cha Kasekese na Kituo cha Afya cha Mwese kuna tatizo kubwa la ukosefu wa Jengo la Mama na Mtoto, Maabara na nyumba za watumishi. Je, ni lini Serikali itapeleka fedha,ili iweze kukamilisha hivyo vituo vya afya? Ahsante.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. JAFAR R. SEIF): Mheshimiwa Naibu Spika, kama nilivyosema awali kwamba, zaidi ya vituo 532 vimeishatengewa bajeti ya shilingi bilioni 102.08. Kwa hiyo, pamoja na vituo ambavyo Mheshimiwa Mbunge ameviainisha vimo katika ukarabati huu mkubwa na kuweza kujenga majengo mengine ambayo yanahitaji, kama maabara, ili kuendelea kupata huduma kwa wananchi wetu.