MHE. SARA M. ALLY: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi hii ya kuuliza swali la nyongea. Jimbo la Mvomero lina miradi sita ya maji inayoendelea ambayo imekuwa ikisuasua kutokana na changamoto za kifedha ikiwepo Mradi wa Maji wa Tandale - Homboza na Mradi wa Dakawa. Je, lini Serikali itapeleka fedha ili hii miradi sita ikamilike kwa wakati na wananchi waweze kupata huduma? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ninapenda kujibu swali la nyongeza la dada yangu Mheshimiwa Sara Msafiri, Mbunge wa Mvomero, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, nilifanya ziara kwenye Jimbo la Mvomero na Mradi huu wa Dakawa pamoja na Tandale ni kweli kabisa kwamba ni mkombozi kwa wananchi wa Mvomero utakapokamilika, lakini kati ya miradi ambayo 878 inayoendelea yenye gharama ya shilingi trilioni 1.3 na hii miradi iko humu. Nimtoe hofu Mheshimiwa Mbunge, maelekezo ya Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan ni kuhakikisha miradi viporo vyote inaisha ili wananchi waweze kuona matokeo na maji yatoke kwa ajili ya matumizi ya maji safi na salama. Ninakushukuru sana. (Makofi)