Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions from Hon. Masanja Kungu Kadogosa (1 total)

MHE. MASANJA K. KADOGOSA: Mheshimiwa Spika, ninakushukuru kwa kunipa hii fursa. Serikali ilifanya tathmini ya uwanja wetu wa Simiyu eneo la lgegu na hiyo tathmini ilifanyika kwa takribani miaka minne iliyopita. Je, ni lini sasa Serikali itatoa fidia lakini vilevile kuanza ujenzi wa uwanja ule?
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mshimwa Spika, ninampongeza Mshimiwa Kadogosa kwa kufuatilia Uwanja wa Ndege wa Mkoa wa Simiyu kwa sababu pia ni sera za Serikali kuhakikisha kwamba angalau kila mkoa unaweza kupata uwanja wa ndege.

Mheshimiwa Spika, nimhakikishie Serikali imeshakamilisha usanifu wa uwanja huo na tumebaini kwamba tunahitaji eka karibu 3,386 na wananchi 700 kama na 92 ambao tumewatambua pale kiasi wanachodai ni shilingi bilioni 6.2. Nimwombe avumilie. Mara baada ya upatikanaji wa fedha tutaweza kwenda kulipa eneo hilo. (Makofi)