Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions from Hon. Abubakar Alli Omari (1 total)

MHE. ABUBAKAR A. OMARI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa nafasi hii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wananchi wangu wa maeneo ya Jimbo la Manonga ambao wameshafikiwa na mradi wa maji ya Ziwa Victoria, lakini upatikanaji wake imekuwa ni matatizo makubwa sana. Inapita mpaka wiki mbili, tatu maji haijatoka. Kuna shule ya sekondari iko Ntigu maeneo ya Ntigu, Usongo, wanafunzi imebidi waondoke kwa kukosa maji.

Je, Serikali ina mipango gani wa kuhakikisha maji ambayo yamekuja kwa gharama kubwa sana ya Serikali na yanapatikana kwa wananchi? (Makofi)

MWENYEKITI: Mheshimiwa Abubakar Omari tafadhali rudia swali lako na isogelee microphone. Sogelea kipaza sauti Mheshimiwa.

MHE. ABUBAKAR A. OMARI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nasema hivi; wananchi wangu wa Jimbo la Manonga maeneo ambayo Mradi wa Maji ya Ziwa Victoria yamefika, lakini maji hayatoki mpaka wiki mbili mpaka tatu kiasi kwamba watu sasa hivi ukiwatajia Mradi wa Maji ya Ziwa Victoria maeneo yale, wanakuwa yaani hawakuelewi. Kwa mfano, sasa hivi kuna wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Seif Gulamali wameanza kuondoka shuleni kwa kukosa maji wiki ya pili mpaka tatu sasa hivi. Shida ni nini hasa?


NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninapenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Abubakar; jambo ambalo ameliongea ni jambo ambalo ni zito kidogo na ni la msingi sana. Wananchi ama wanafunzi kutoka shuleni ama kuondoka shuleni kwa sababu ya kukosa huduma ya maji safi na salama, si utaratibu na wala siyo maelekezo ya Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan. Baada ya kikao hiki cha Bunge Mheshimiwa Mbunge tuonane ili tuende kuhakikisha kwamba tunachukua hatua za haraka ili wananchi na wanafunzi wa shule hiyo wanapata huduma ambayo inatarajiwa. Ahsante sana. (Makofi)