Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions from Hon. Juma Ramadhani Mustafa (1 total)

MHE. JUMA R. MUSTAFA: Mheshimiwa Spika, ninashukuru kwa majibu mazuri ya Wizara. Kwanza kabisa ninapenda kuwapongeza kwa kazi nzuri ambazo wanaendelea kuzifanya, lakini ninampongeza Mheshimiwa Rais, wananchi wa Jimbo la Igalula wanamshukuru kwenye chanjo ya ruzuku, kuondoa na utambuzi wa mifugo.
Mheshimiwa Spika, nina swali moja la nyongeza; je, Serikali ina utaratibu gani wa kisheria na kiutendaji, ili kuhakikisha sasa maeneo haya yaliyotengwa hayavamiwi na hayabadilishiwi matumizi ili kuweza kuepuka migogoro kati ya wakulima na wafugaji ndani ya Jimbo la Igalula?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. RAJAB S. JAFAR): Mheshimiwa Spika, ninapenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Juma Mustafa Kawamba, Mbunge wa Igalula, Halmashauri ya Uyui, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kumekuwa na Sheria mbalimbali ambazo zimekuwa zikitu-guide na zimepitishwa na Bunge lako Tukufu. Sheria ya Ardhi ya Mwaka 1999, hii ilikuwa inatoa hati ya Hatimiliki ya Kimila, lakini kuna Sheria ya Ardhi Namba Sita ya Mwaka 2007, ambayo imeainisha mipango ya matumizi ya ardhi ya vijiji, lakini kuna maeneo ya kilimo na malisho ya mifugo, yote yameainishwa katika Sheria hii. Sambamba na sheria hizi pia, kuna Sheria Namba 287, ambayo imewezesha halmashauri kutunga Sheria Ndogo. Kwa hiyo, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, TAMISEMI, ninaziagiza Halmashauri zote nchini zifuatishe Sheria hizi na kuona zinatatua migogoro ya ardhi katika maeneo yao.