MHE. ENG. AMOSY W. MAGANGA aliuliza:-
Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga Barabara ya Ipole – Rungwa na Sikonge – Kipili kwa kiwango cha lami?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, ninaomba kujibu swali la Mheshimiwa Engineer Amos William Maganga, Mbunge wa Sikonge, kama ifuatavyo: -
Mheshimiwa Naibu Spika, upembuzi yakinifu na usanifu wa kina kwa ajili ya ujenzi kwa kiwango cha lami wa Barabara ya Ipole – Rungwa inayounganisha Mikoa ya Tabora na Mbeya umekamilika. Kwa sasa Serikali inaendelea kutafuta fedha kwa ajili ya kuanza ujenzi wa barabara hiyo.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu Barabara ya Sikonge – Kipili Serikali inaendelea kutafuta fedha kwa ajili ya kuifanyia upembuzi yakinifu na usanifu wa kina kwa ajili ya kuijenga kwa kiwango cha lami. Baada ya Usanifu kukamilika, Serikali itatafuta fedha kwa ajili ya kuanza ujenzi. Ahsante.