Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Questions from Hon. Charles Mhando Njama (1 total)

MHE. CHARLES M. NJAMA aliuliza:-

Je, lini barabara ya Old Korogwe – Kwamndolwa kilomita 10 itajengwa kwa kiwango cha lami?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, ninapenda kujibu swali la Mheshimiwa Charles Mhando Njama, Mbunge wa Korogwe Mjini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Barabara ya Old Korogwe ni sehemu ya barabara ya Mkoa ya Old Korogwe – Kwamndolwa – Magoma – Mashewa – Bombomtoni – Mabokweni yenye urefu wa kilometa 127.69. Mradi wa ujenzi kwa kiwango cha lami kwa sehemu ya Old Korogwe – Kwamndolwa yenye urefu wa kilomita 10 upo katika hatua ya manunuzi kwa ajili ya kumpata Mkandarasi. Mara baada ya kumpata Mkandarasi ujenzi kwa kiwango cha lami utaanza. Ahsante.