Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions from Hon. Bakari Bakari Shingo (1 total)

MHE. BAKARI B. SHINGO: Mheshimiwa Spika, ninashukuru sana kwa kunipa nafasi hii na nina swali dogo la nyongeza. Katika Jimbo langu la Ukonga, hasa Halmashauri yetu Jiji la Dar es Salaam moja ya mambo yaliyopelekea halmashauri ikahamisha utaratibu wa kukopesha moja kwa moja ni baadhi ya watumishi wa halmashauri na baadhi ya Madiwani walisemwa kwamba wamekuwa wakitumia mlango wa nyuma kujikopesha, lakini pia kuwepo na vikundi ambavyo sasa vimekopeshwa zaidi ya mamilioni na vimetajwa kuwa havionekani.

Mheshimiwa Spika, swali langu ni kuwa; je, kwa ajili ya kulinda maslahi mapana ya Taifa na kodi zetu, ni kwa nini Serikali isiweke utaratibu wa kuyataja hadharani hayo makundi ama hivyo vikundi vilivyokopa ambavyo sasa havionekani, sambamba na baadhi ya watumishi wa halmashauri ambao siyo waaminifu waolijingiza katika mtego huu ambao leo unapelekea halmashauri zetu kuhamisha Mfuko huo kupeleka kwenye benki, benki ambazo zinasababisha tushindwe kupata mikopo?
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Spika, pamoja na majibu mazuri ambayo Naibu wangu ameyatoa, kama alivyosema, tulikuwa na kikao na benki hizi. Kilichotokea ni kwamba, kweli kwenye majiji kuna fedha nyingi ambazo hazijakopeshwa uki-compare na kwenye halmashauri za wilaya na miji. Shida iliyopo, kutokana na maelezo waliyotupa benki; la kwanza, ni kweli kwamba walikuwa na masharti magumu, lakini kwa sasa sharti linalotakiwa kwa mtu kwa kikundi kukopa ni wale wanakikundi kuwa na NIDA.
Mheshimiwa Spika, nini kimesababisha sasa majiji yawe na fedha nyingi; wamesema, ni kwa sababu wale wanaounda vikundi walioko Dar es Salaam kwa mfano wanakutana kimjini mjini, kwa hiyo hawawezi na inakuwa ngumu sana kupata kikundi kimoja cha watu ambao wanaweza kukopeshwa kwa wakati huo. Hii ni kwa sababu, huyu ametoka Segerea, mwingine ametoka Ubungo, mwingine tena ametoka Kawe na wanakutana Kariakoo kwenye biashara. Wakiwa pale kila mtu hajui huyo mwenzake ametokea wapi.

Mheshimiwa Spika, proposal ya benki ni kwamba, ikiwezekana tuwape mikopo individuals kama tunavyofanya kwa walemavu; lakini tuwe na condition moja kwamba huyu individual tunayempa mkopo atuhakikishie kwamba kwanza ana biashara, ana leseni ya biashara; lakini pili, ataweza ku-employ angalau watu watatu kwenye ile biashara kutokana na mkopo tunaowapa.

Mheshimiwa Spika, kama hii itafanyika, kitu cha kwanza zile bilioni zilizolala kule benki zitatoka. Kitu cha pili, tutaona kwamba tume-create ajira kwa vijana ambao ni moja ya vitu ambavyo tunaviangalia sana kwenye fedha hii. Kwa hiyo Bunge lako hili ninaomba lielewe kwamba, tutakwenda kuona namna ya kubadilisha ule mwongozo na kukubali kwamba tuwe na pilot ya majiji ya kutoa mikopo kwa individuals ambao watatuhakikishia kwamba wata-create ajira kwenye maeneo haya.

Mheshimiwa Spika, nimeomba nisimame nitoe ufafanuzi huu na kushukuru sana.