MHE. JAFARI W. CHEGE: Mheshimiwa Naibu Spika, ninakushukuru kwa kunipa nafasi. Nimpongeze Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu mazuri, lakini nina swali la nyongeza. Mradi wa Maji wa Miji 28 Rorya, Tarime umesimama kwa muda mrefu na Mheshimiwa Naibu Waziri atakubaliana nami mradi ule umekwenda kwa kusuasua sana kwa muda mrefu kwa sababu ya ukosefu wa fedha. Je, ni lini Serikali itapeleka fedha kwa ajili ya ukamilishaji wa mradi huo.
NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ninapenda kujibu swali la Mheshimiwa Jafari Chege, Mbunge wa Rorya, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kabisa Mradi huu wa kutoka Tarime – Rorya ambao awali tulitegemea mradi huu pia ukatoe huduma maeneo ya Serengeti, Mugumu kule ni kweli umesuasusa. Hata hivyo, Wizara tumechukua hatua ya kukaa na Wakandarasi wakati Serikali ikiendelea kutafuta fedha. Mradi huu Mkandarasi aendelee kuutekeleza ili lengo ni kwamba atakapokuwa ana-raise certificate, basi Serikali itaweza kumlipa kulingana na kazi atakayokuwa ameifanya. Ninakushukuru sana.