MHE. YOHANA S. MSITA aliuliza:-
Je, nini mpango wa Serikali wa kupandisha bei ya zao la dengu baada ya bei kuporomoka?
NAIBU WAZIRI WA KILIMO alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imeanza kutekeleza Mkakati wa kusambaza mbegu bora za dengu nchini ambapo katika mwaka wa fedha 2025/2026, Wizara imepanga kusambaza kilo 400 za mbegu mama za dengu kwa wakulima wa Halmashauri ya Itigi zenye uwezo wa kuzalisha tani nne za mbegu bora. Lengo ni kuhakikisha wakulima wanaongeza tija na uzalishaji ili kukidhi mahitaji ya soko la kimataifa na kuwawezesha wakulima kupata bei nzuri.
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali vilevile inaendelea na taratibu za kufungua soko la dengu Nchini Malaysia. Upatikanaji wa soko hilo utaruhusu zao la dengu kuingia rasmi katika soko la Malaysia. Hatua hiyo itaongeza wigo wa masoko na hivyo kuimarisha bei kwa mkulima.