Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions from Hon. Asha Juma Feruz (1 total)

MHE. ASHA J. FERUZ: Mheshimiwa Mwenyekiti, jina langu ni
Asha Juma Feruz, Mwakilishi ninayewakilisha kundi la Vyuo Vikuu.
Ninaomba kuuliza swali la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, je, Serikali ina mkakati gani
maalumu katika kutumia fursa za ajira katika kundi la vyuo na
vyuo vikuu kupitia mahusiano ya kikanda na kidiplomasia
tuliyonayo hasa zile kozi tunazoziita rare professionals? (Makofi)
NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, AJIRA NA
MAHUSIANO (MHE. RAHMA R. KISUO): Mheshimiwa Mwenyekiti,
Serikali kwa kushirikiana na vyuo na vyuo vikuu, imeanzisha
mafunzo kwa vitendo kwa wanafunzi wanaoendelea na masomo
katika ngazi mbalimbali za elimu za vyuo na vyuo vikuu na vyuo
vya kati ikiwa ni sehemu ya mtaala ili kuwawezesha kuhitimu elimu
katika ngazi hizo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile, Serikali inatoa Mafunzo ya
Internship yanayojumuisha wahitimu wa ujuzi wa ngazi mbalimbali
za elimu hususan elimu ya juu na kati ambapo wanapatiwa fursa
ya kujifunza kwa vitendo mahali pa kazi. Lengo la mafunzo hayo
ni kuwapatia wahitimu ujuzi, maadili ya kazi, uzoefu na kufanya
kazi za taaluma zao na kuwawezesha kuajirika. (Makofi)