Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions from Hon. Josephine Joseph Kapoma (2 total)

MHE. JOSEPHINE J. KAPOMA: Je, Wizara ina mkakati gani wa kuja na solution ya kudumu, na hata kama siyo ya kudumu japokuwa ya muda mrefu kwa zile barabara zinazozibwa viraka? Kwa mfano, kuna baadhi ya barabara unakuta zina mashimo, lakini zinazibwa mara kwa mara.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nilikuwa ninataka kujua kama tunaweza tukapata solution ya kuziba viraka ambavyo vitakaa kwa muda mrefu kwa ajili ya ku-save pesa ambazo zinatumika. (Makofi)



NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. KWAGILWA R. NHAMANILO): Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimpongeze Mbunge wa Mkoa mzima wa Morogoro aliyetoka kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan ametupa maelekezo sisi TARURA ndani ya Serikali kwa ajili ya kuanza mkakati wa kutumia teknolojia mpya ambayo itajenga barabara zetu kwa gharama nafuu na hivyo tutaweza kuyafikia maeneo mengi na kujenga barabara zinazodumu kwa muda mrefu zaidi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa huu Mkoa wa Morogoro ambao Wabunge wake wameuliza maswali mengi hapa, Mheshimiwa Rais amefanya kazi kubwa sana, tumejenga mtandao wa barabara kwa kiwango cha lami na sasa tumefikisha karibia kilometa 125. Mradi wa TACTIC ambao tulitekeleza kwa awamu ya kwanza tulipeleka zaidi ya shilingi bilioni 19. Mheshimiwa Rais lengo lake ni kutaka kuona anaufungua Mkoa huu mkubwa ambao ni muhimu kwa uchumi ndani ya nchi yetu. (Makofi)
MHE. JOSEPHINE J. KAPOMA: Mheshimiwa Naibu Spika, nilikuwa nina swali dogo la nyongeza. Kama ikimpendeza Mheshimiwa Naibu Waziri atalijibu au atalichukuwa. Wilaya yetu ya Malinyi tumekuwa tuna shida ya gereza la mahabusu kwa muda mrefu sana. Eneo limepatikana lakini kumekuwa kuna ucheleweshwaji wa kukamilisha ambayo inawafanya wahusika kusafiri umbali mrefu sana kwenda Wilaya ya Ulanga. Je, Serikali ina mpango gani wa kukamilisha suala hili? Ahsante.
NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, ninaomba nimfahamu ili niweze kujibu vizuri; amekusudia mahabusu ya polisi au ya gereza?NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Mbunge.

MHE. JOSEPHINE J. KAPOMA: Mheshimiwa Naibu Spika, mahabusu ya gereza.

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, tulikuwa tunaongelea kuhusu suala la Jeshi la Polisi lakini kwa sababu Magereza na yenyewe ni sehemu ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, lakini ninaomba tu nimjibu Mheshimiwa Kapoma kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli yapo baadhi ya magereza yamekuwa na changamoto ya uchakavu wa majengo. Hata hivyo, moja ya eneo ambalo amelitaja la jimbo lake kwamba wilaya nzima ya Malinyi hakuna gereza na kupeleka eneo la pili; tunakuja na mpango na tutaueleza kwenye bajeti ya mwaka huu kwamba ni mpango gani kwa upande wa Jeshi la Magereza, tutaenda kuboresha magereza katika maeneo ambayo yana uhaba likiwepo eneo lake la Malinyi.