Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions from Hon. Khalid Mussa Nsekela (1 total)

MHE. KHALID M. NSEKELA: Mheshimiwa Spika, kwanza ninaungana na wenzangu kumtakia heri ya kuzaliwa Rais wetu, Dkt. Samia Suluhu Hassan. Ninaishukuru Serikali kwa kutuletea mkandarasi wa kujenga Barabara ya lami kutoka Kyerwa kwenda Omurushaka, kilometa 50. Hata hivyo, speed yake ni ndogo sana. Je, Serikali ina mkakati na maelekezo gani ya kumsimamia mkandarasi huyu ili amalize barabara hii ili kukidhi kilio cha wananchi wa Kyerwa? Ninakushukuru sana.
NAIBU WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Spika, ninaomba kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli mkandarasi huyu anakichofanya ni sanifu jenga Barabara ya Kyerwa kwenda Omurushaka. Nimwagize Meneja na Mhandisi Mshauri anayemsimamia ahakikishe kwamba huyu mkandarasi, kwa sababu alikwishalipwa fedha ya awali, aweze kwenda kwa kasi inayotakiwa kulingana na mpango wake wa kazi ambao ameupanga na tumeukubali. (Makofi)