Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2020-2025 | Session 19 | Sitting 50 | Regional Administration and Local Government Authorities | Ofisi ya Rais TAMISEMI. | 636 | 2025-06-20 |
Name
Nicholaus George Ngassa
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Igunga
Primary Question
MHE. NICHOLAUS G. NGASSA aliuliza: -
Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara kwa kiwango cha lami kuunganisha kipande cha Mbutu na Igunga Mjini?
Name
Zainab Athuman Katimba
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. ZAINAB A. KATIMBA) alijibu: -
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inatambua umuhimu wa kipande cha barabara ya Mbutu hadi Igunga Mjini chenye urefu wa kilometa tano na imepanga kufanya usanifu wa kina katika mwaka wa fedha 2025/2026. Hatua hii inalenga kubaini gharama halisi za ujenzi, mahitaji ya kiufundi na kuandaa nyaraka za zabuni zitakazotumika wakati wa utekelezaji wa mradi huu.
Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kukamilika kwa usanifu huo, Serikali imepanga kuanza utekelezaji wa ujenzi wa barabara hii kwa kiwango cha lami kuanzia mwaka wa fedha 2026/2027 kulingana na upatikanaji wa fedha.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved