Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2025-2030 | Session 2 | Sitting 5 | Regional Administration and Local Government Authorities | Ofisi ya Waziri Mkuu-Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) | 72 | 2026-02-02 |
Name
Paschal Inyasi Chinyele
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Dodoma mjini
Primary Question
MHE. PASCHAL I. CHINYELE aliuliza:-
Je, kwa nini wananchi wa Kata ya Mbalawala wamezuiwa kuendeleza ardhi wanayomiliki kwa maelezo kuwa ni sehemu ya Bonde la Kati Singida?
Name
Dr. Jafar Rajab Seif
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Busanda
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. JAFAR R. SEIF) alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, ninaomba kujibu swali la Mheshimiwa Paschal Inyasi Chinyele, Mbunge wa Dodoma Mjini. Bonde la Mzakwe linasimamiwa na Mamlaka ya Bonde la Wami Ruvu Water Basin na Mamlaka ya DUWASA na siyo Bonde la Kati la Singida kama swali lilivyoelekezwa. Bonde hili lilipimwa kisheria na kusajiliwa Aprili, 2000 kwa ramani yenye Namba 45977.
Mheshimiwa Naibu Spika, eneo hilo lina ukubwa wa hekta zaidi ya 34,000 na lipo katika Kata za Chihikwi, Kawawa, Matangizi, Makulu na Mtaa wa Muungano.
Mheshimiwa Naibu Spika, sababu zilizopelekea kuzuiwa kufanya maendelezo katika bonde hilo ni kuhifadhi vyanzo vya maji kwa kuwa kuna zaidi ya visima 20 vinavyotoa huduma ya maji yanayotumika na wananchi wa Dodoma Mjini na maeneo jirani, eneo ilo kitaalam lina kimo cha maji kilichopo juu. Serikali imechukua hatua za kusitisha upimaji na umilikishaji pamoja na kuendelea kutoa elimu kwa wananchi juu ya athari ya kuendeleza eneo hilo.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved