Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2025-2030 Session 2 Sitting 5 Works and Transport Wizara ya Ujenzi 80 2026-02-02

Name

Janeth Peter Pinda

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JANETH P. PINDA aliuliza:-

Je, Serikali ina mpango gani wa kukamilisha ujenzi wa Barabara ya kutoka Wilaya ya Tanganyika hadi Uvinza?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, ninapenda kujibu swali la Mheshimiwa Janeth Peter Pinda, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, ujenzi wa barabara hii unatekelezwa kwa awamu ambapo ujenzi kwa sehemu ya kwanza ya Mpanda – Vikonge kilomita 37.65 umekamilika. Ujenzi wa sehemu ya pili ya Vikonge – Luhafwe kilomita 25 unaendelea na umefikia 70% na ujenzi wa sehemu ya tatu ya Luhafwe – Mishamo kilomita 37.35 unaendelea na umefikia 30.6%. Kwa sehemu iliyobaki ya Mishamo – Uvinza urefu kilomita 95.6, Serikali inaendelea kutafuta fedha kwa ajili ya kuanza ujenzi. Ahsante.