Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2025-2030 | Session 2 | Sitting 5 | Works and Transport | Wizara ya Ujenzi | 80 | 2026-02-02 |
Name
Janeth Peter Pinda
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. JANETH P. PINDA aliuliza:-
Je, Serikali ina mpango gani wa kukamilisha ujenzi wa Barabara ya kutoka Wilaya ya Tanganyika hadi Uvinza?
Name
Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Ileje
Answer
NAIBU WAZIRI WA UJENZI alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, ninapenda kujibu swali la Mheshimiwa Janeth Peter Pinda, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, ujenzi wa barabara hii unatekelezwa kwa awamu ambapo ujenzi kwa sehemu ya kwanza ya Mpanda – Vikonge kilomita 37.65 umekamilika. Ujenzi wa sehemu ya pili ya Vikonge – Luhafwe kilomita 25 unaendelea na umefikia 70% na ujenzi wa sehemu ya tatu ya Luhafwe – Mishamo kilomita 37.35 unaendelea na umefikia 30.6%. Kwa sehemu iliyobaki ya Mishamo – Uvinza urefu kilomita 95.6, Serikali inaendelea kutafuta fedha kwa ajili ya kuanza ujenzi. Ahsante.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved