Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2025-2030 Session 2 Sitting 5 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Wizara ya Kilimo 84 2026-02-02

Name

Shaffin Ahmedali Sumar

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uyui

Primary Question

MHE. SHAFFIN A. SUMAR aliuliza:-

Je, Serikali inawasaidiaje wakulima wa tumbaku kupitia AMCOS kulipwa fedha jumla ya dola milioni 1.2 wanazodai kwenye kampuni?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Katika msimu wa 2024/2025 wakulima wa tumbaku waliuza kilo milioni 185.7 zenye thamani ya dola za Marekani milioni 475.45. Kati ya kiasi hicho, dola za Marekani milioni 470.95 sawa na 99.05% zimeshalipwa. Aidha, kiasi kinachodaiwa ni dola za Marekani Milioni 4.51 sawa na 0.95%. Kati ya kiasi kinachodaiwa, dola za Marekani 298,007.23 ni kutoka Wilaya ya Uyui.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inaendelea kufuatilia madai ya wakulima wote wa zao la tumbaku ikiwemo wakulima kutoka Wilaya ya Uyui ili kuhakikisha madai yote ya wakulima wa zao la tumbaku hiyo yanalipwa kabla ya mwezi Machi, 2026.