Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2025-2030 | Session 2 | Sitting 5 | Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives | Wizara ya Kilimo | 84 | 2026-02-02 |
Name
Shaffin Ahmedali Sumar
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Uyui
Primary Question
MHE. SHAFFIN A. SUMAR aliuliza:-
Je, Serikali inawasaidiaje wakulima wa tumbaku kupitia AMCOS kulipwa fedha jumla ya dola milioni 1.2 wanazodai kwenye kampuni?
Name
David Ernest Silinde
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Tunduma
Answer
NAIBU WAZIRI WA KILIMO alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Katika msimu wa 2024/2025 wakulima wa tumbaku waliuza kilo milioni 185.7 zenye thamani ya dola za Marekani milioni 475.45. Kati ya kiasi hicho, dola za Marekani milioni 470.95 sawa na 99.05% zimeshalipwa. Aidha, kiasi kinachodaiwa ni dola za Marekani Milioni 4.51 sawa na 0.95%. Kati ya kiasi kinachodaiwa, dola za Marekani 298,007.23 ni kutoka Wilaya ya Uyui.
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inaendelea kufuatilia madai ya wakulima wote wa zao la tumbaku ikiwemo wakulima kutoka Wilaya ya Uyui ili kuhakikisha madai yote ya wakulima wa zao la tumbaku hiyo yanalipwa kabla ya mwezi Machi, 2026.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved