Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2025-2030 Session 2 Sitting 5 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Wizara ya Kilimo 85 2026-02-02

Name

Alan Thomas Mvano

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kakonko

Primary Question

MHE. ALAN T. MVANO aliuliza:-

Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha wakulima wa zao la muhogo Kakonko wanapata soko la uhakika?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali kwa kushirikiana na sekta binafsi imeendelea kutekeleza mkakati wa kuendeleza zao la muhogo nchini kwa lengo la kuongeza tija na uzalishaji, kuimarisha upatikanaji wa masoko ya uhakika ya bidhaa za muhogo na kuhamasisha uwekezaji wa viwanda vya kuchakata muhogo ili kuongeza thamani ya zao hilo. Moja ya eneo la kimkakati katika kuendeleza muhogo ni Halmashauri za Wilaya ya Kakonko na Kibondo, Mkoani Kigoma.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali katika mwaka wa fedha 2025/2026, imetenga fedha kwa ajili ya kujenga miundombinu ya masoko, kukaushia, kuchakata na kuhifadhi muhogo katika Halmashauri ya Kakonko. Tayari Wizara imefanya tathmini ya eneo kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu hiyo pamoja na kuandaa usanifu, michoro na gharama za awali kwa ajili ya kuanza kumtafuta mkandarasi wa ujenzi. Wizara inaamini taratibu zote zitakamilika mapema ili kuhakikisha wakulima wanaanza kuongeza thamani ya zao la muhogo, kupunguza upotevu baada ya mavuno na kuimarisha upatikanaji wa masoko kwa wakulima. Ahsante sana.