Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2025-2030 Session 2 Sitting 9 Education, Science,Technology and Vocational Training, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia 144 2026-02-06

Name

Thomas Maganga Kampala

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Katavi

Primary Question

MHE. THOMAS K. MAGANGA aliuliza:-

Je, lini Serikali itakamilisha ujenzi wa Chuo cha VETA Halmashauri ya Wilaya ya Mlele – Katavi?

Name

Omari Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa ruhusa yako na kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, ninaomba nijibu swali la Mheshimiwa Thomas Kampala Maganga, Mbunge wa Katavi, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali inaendelea na ujenzi wa Chuo cha VETA cha Wilaya ya Mlele ambacho kinatarajiwa kukamilika mwezi Juni, 2026. Hadi sasa Serikali imeshatumia jumla ya Shilingi Bilioni 1.032 kati ya Shilingi Bilioni 1.6 zilizotengwa kwa ajili ya kukamilisha ujenzi wa awamu ya kwanza. Mpaka sasa, ujenzi huo umefikia 73%.

Mheshimiwa Spika, Serikali itaendelea kutenga na kupokea fedha ili kuwezesha ujenzi wa chuo hiki kukamilika kwa wakati na kuanza kutoa mafunzo kama ilivyopangwa.