Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2025-2030 | Session 3 | Sitting 32 | Regional Administration and Local Government Authorities | Ofisi ya Waziri Mkuu-Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) | 373 | 2026-05-19 |
Name
Devotha Daniel Mburarugaba
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. DEVOTHA D. MBURARUGABA aliuliza:-
Je, Serikali ina mpango gani kuhakikisha Wabunge wa Viti Maalum wanashirikishwa katika utoaji wa mikopo ya 10% kwenye halmashauri?
Name
Dr. Festo John Dugange
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Wanging'ombe
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, TAMISEMI, ninaomba kujibu swali la Mheshimiwa Devotha Daniel Mburarugaba, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inatatanrmbua umuhimu wa kuwashirikisha Waheshimiwa Wabunge wote wakiwemo wa Viti Maalum, katika utoaji na usimamizi wa mikopo ya 10% katika halmashauri. Kufuatia maboresho ya sheria, kanuni na mwongozo wa utoaji na usimamizi wa mikopo hiyo wa mwaka 2024, Serikali imeweka utaratibu wa ushirikishwaji wa Waheshimiwa Wabunge kuhusu hatua za utoaji mikopo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, chini ya utaratibu huo, Waheshimiwa Wabunge wanatakiwa washirikishwe kikamilifu kupitia vikao vya kisheria vya halmashauri, hususani Baraza la Madiwani na Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango ambapo hupokea taarifa, kujadili na kutoa maoni kuhusu upangaji, ugawaji na usimamizi wa mikopo ya 10% kwa wanawake, vijana na watu wenye ulemavu.
Aidha, Ofisi ya Waziri Mkuu, TAMISEMI imewaelekeza Wakurugenzi wa Mamlaka za Serikali za Mitaa kuwataarifu na kuwaalika Waheshimiwa Wabunge kushiriki kwenye shughuli za utoaji mikopo katika halmshauri zao ili kuwapa fursa ya kuhamasisha, kuelimisha na kufuatilia shughuli za vikundi kutokana na mikopo hiyo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inazisistiza halmashauri zote nchini kuendelea kuimarisha utaratibu wa mawasiliano na kuwapa taarifa kwa wakati Waheshimiwa Wabunge kuhusu ratiba za vikao, orodha ya wanufaika na mwenendo wa urejeshaji wa mikopo ili kuongeza uwazi na uwajibikaji. Ahsante.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved