Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2025-2030 | Session 3 | Sitting 14 | Education, Science,Technology and Vocational Training, | Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia | 164 | 2026-04-22 |
Name
Dr. Regina Christopher Malima
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. DKT. REGINA C. MALIMA aliuliza:-
Je, Serikali imejipangaje kuboresha Programu za Uanagenzi, Ufundi Stadi na Ubunifu ili kuwawezesha Vijana kujiajiri na kuondoa changamoto ya ajira?
Name
Wanu Hafidh Ameir
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Answer
NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa ruhusa yako na kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, naomba nijibu swali la Mheshimiwa Dkt. Regina Christopher Malima kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kupitia Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA) imeendelea kueneza Mpango wa Mafunzo kwa Mfumo wa Uanagenzi Pacha (Dual Apprenticeship Training System) ambapo mafunzo yanatolewa kwa kushirikiana na viwanda. Mfumo huu unaendeshwa kwa utaratibu Ungwe (Block Release) ambapo wanafunzi hujifunza kwa kubadilishana muda wa kuwa chuoni kisha viwandani na sehemu za kazi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mfumo huu unawawezesha wanafunzi kupata umahiri kwa haraka na fursa za ajira pindi wanapohitimu. Kwa sasa mfumo wa DATS unatumika kwa fani za kilimo, ukarimu, utalii, ufundi magari, ufundi umeme na programu za madini.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imeandaa mikakati ikiwa ni pamoja na kuimarisha ushirikiano na viwanda na waajiri; kujenga uelewa kwa wadau wa viwanda (Industrial Mentors) na kueneza mfumo wa DATS kwa kuongeza fani za mafunzo na Vyuo.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved