Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2025-2030 | Session 3 | Sitting 19 | Regional Administration and Local Government Authorities | Ofisi ya Waziri Mkuu-Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) | 218 | 2026-04-29 |
Name
Aisha Msantu Mduyah
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. AISHA M. MDUYAH aliuliza:-
Je, Serikali ina mkakati gani wa kuwawekea Miundombinu wezeshi Wanafunzi wenye mahitaji maalum ili wasome fani wanazozipenda?
Name
Dr. Festo John Dugange
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Wanging'ombe
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, TAMISEMI, ninaomba kujibu swali la Mheshimiwa Aisha Msantu Mduyah, Mbunge wa Viti Malaam, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa mujibu wa Mwongozo wa Utekelezaji wa Mkakati wa Elimu Jumuishi wa mwaka 2022 - 2026 na Waraka Namba Tatu wa mwaka 2025 kuhusu mfumo wa Kitaifa wa kuzifanya shule kuwa Jumuishi mwelekeo wa Serikali ni kuzifanya shule zote za msingi na sekondari zilizopo kuwa jumuishi.
Mheshimiwa Naibu Spika, mkakati wa Serikali kuzifanya shule za msingi na sekondari kuwa jumuishi, ni pamoja na kuhakikisha kuwa miundombinu inayojengwa inakuwa rafiki kwa wanafunzi wenye mahitaji maalum, kuhakikisha kuwa bajeti ya Serikali inajumuisha fedha ya ununuzi wa vifaa wezeshi na vifaa visaidizi kwa watoto wenye mahitaji maalum, kutoa ajira kwa walimu wa wanafunzi wenye mahitaji maalumu na kutoa mafunzo kwa walimu wa elimu maalum.
Mheshimiwa Naibu Spika, hadi sasa kuna shule maalum 44 za msingi na moja ya sekondari, vitengo maalumu 815 kwa shule za msingi na shule za awali na msingi jumuishi 20,889 na sekondari ni 6488. Vilevile, shule jumuishi 53 za sekondari za bweni Kitaifa na tatu za kutwa zinapokea wanafunzi wenye mahitaji maalumu ambao wana changamoto kubwa zaidi nchi nzima. Serikali itaendelea kuboresha shule za msingi na sekondari ili ziwe jumuishi zaidi kwa wanafunzi wenye mahitaji maalum, ahsante. (Makofi)
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved