Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2025-2030 | Session 3 | Sitting 18 | Information, Communication and Information Technology | Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari | 212 | 2026-04-28 |
Name
Edibily Kinyoma Kazala
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Kasulu Vijijini
Primary Question
MHE. EDIBILY K. KINYOMA aliuliza: -
Je, lini Serikali itamaliza changamoto ya Mawasiliano kwa kujenga Minara Kata za Heru Ushingo, Kagerankanda na Asante Nyerere - Kasulu Vijijini?
Name
Switbert Zacharia Mkama
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Ukerewe
Answer
NAIBU WAZIRI WA MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI alijibu: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, ninaomba kujibu swali la Mheshimiwa Edibily Kazala Kinyoma, Mbunge wa Jimbo la Kasulu Vijijini, kama ifuatavyo: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kupitia Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote – UCSAF ilikamilisha ujenzi wa Mnara Mwaka 2014 kupitia Kampuni ya Honora au (Yas Tanzania) kwa ajili ya kuhudumia Vijiji vya Seruhemebe na Heru vilivyopo katika Kata ya Heru Ushingo. Aidha, katika Kata za Kagerankanda, UCSAF ilijenga Mnara mwaka 2021 katika Kijiji cha Mvinza kupitia Shirika la Mawasiliano Tanzania.
Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile, katika Kata ya Asante Nyerere, UCSAF ilikamilisha ujenzi wa mnara mwaka 2025 kupitia Kampuni ya Vodacom Tanzania katika Kijiji cha Sogeeni Kwiliba.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na jitihada nilizozitaja awali, Serikali kupitia UCSAF itatuma wataalamu kwenda Kasulu Vijijini katika Kata husika kufanya tathmini ili kujua mahitaji halisi na hatimaye kuviingiza vijiji vyote vyenye changamoto ya mawasiliano katika miradi itakayotekelezwa na UCSAF hususan katika Mpango Mkakati wa Ujenzi wa Minara wa Mwaka 2025 – 2030.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved