Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2025-2030 Session 3 Sitting 18 Information, Communication and Information Technology Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari 212 2026-04-28

Name

Edibily Kinyoma Kazala

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kasulu Vijijini

Primary Question


MHE. EDIBILY K. KINYOMA aliuliza: -

Je, lini Serikali itamaliza changamoto ya Mawasiliano kwa kujenga Minara Kata za Heru Ushingo, Kagerankanda na Asante Nyerere - Kasulu Vijijini?

Name

Switbert Zacharia Mkama

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukerewe

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, ninaomba kujibu swali la Mheshimiwa Edibily Kazala Kinyoma, Mbunge wa Jimbo la Kasulu Vijijini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kupitia Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote – UCSAF ilikamilisha ujenzi wa Mnara Mwaka 2014 kupitia Kampuni ya Honora au (Yas Tanzania) kwa ajili ya kuhudumia Vijiji vya Seruhemebe na Heru vilivyopo katika Kata ya Heru Ushingo. Aidha, katika Kata za Kagerankanda, UCSAF ilijenga Mnara mwaka 2021 katika Kijiji cha Mvinza kupitia Shirika la Mawasiliano Tanzania.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile, katika Kata ya Asante Nyerere, UCSAF ilikamilisha ujenzi wa mnara mwaka 2025 kupitia Kampuni ya Vodacom Tanzania katika Kijiji cha Sogeeni Kwiliba.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na jitihada nilizozitaja awali, Serikali kupitia UCSAF itatuma wataalamu kwenda Kasulu Vijijini katika Kata husika kufanya tathmini ili kujua mahitaji halisi na hatimaye kuviingiza vijiji vyote vyenye changamoto ya mawasiliano katika miradi itakayotekelezwa na UCSAF hususan katika Mpango Mkakati wa Ujenzi wa Minara wa Mwaka 2025 – 2030.