Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2025-2030 | Session 3 | Sitting 6 | Regional Administration and Local Government Authorities | Ofisi ya Waziri Mkuu-Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) | 46 | 2026-04-10 |
Name
Yahya Ally Mhata
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Nanyumbu
Primary Question
MHE. YAHYA A. MHATA aliuliza: -
Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga nyumba za watumishi wa afya ngazi ya kata katika Jimbo la Nanyumbu?
Name
Dr. Jafar Rajab Seif
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Busanda
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. JAFAR R. SEIF) alijibu: -
Mheshimiwa Spika, ninaomba kujibu swali la Mheshimiwa Yahya Ally Mhata, Mbunge wa Jimbo la Nanyumbu, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, TAMISEMI.
Mheshimiwa Spika, Serikali inatambua umuhimu wa kuwa na nyumba za watumishi katika vituo vya kutolea huduma za afya nchini. Kutokana na ongezeko la ujenzi wa vituo vipya, kumepelekea mahitaji makubwa ya nyumba za watumishi.
Mheshimiwa Spika, Serikali imefanya tathmini ya mahitaji ya nyumba za watumishi ambapo jumla ya nyumba 25,690 zinahitajika kote nchini, nyumba za watumishi zilizopo ni takribani 7,696 sawa na 30%. Aidha, katika Halmashauri ya Wilaya ya Nanyumbu takwimu zinaonesha kunahitajika nyumba 147 na zilizopo ni 43 sawa na 29%.
Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2026/2027 Serikali kupitia mapato ya ndani ya Halmashauri ya Wilaya ya Nanyumbu imetenga jumla ya shilingi milioni 100 kwa ajili ya ujenzi wa nyumba mbili za watumishi kwenye Kituo cha Afya Mnanje na Zahanati ya Kazamoyo.
Mheshimiwa Spika, ninaomba kuwasilisha.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved