Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Regina Christopher Malima

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. REGINA C. MALIMA aliuliza:- Je, Serikali imejipangaje kuongeza ajira kwa wahitimu wa vyuo kupitia miradi ya kimkakati, viwanda vidogo, vya kati na programu za ubunifu?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. REGINA C. MALIMA: Mheshimiwa Mwenyekiti,
kwanza kabisa nishukuru kwa majibu mazuri ya Wizara, na
niipongeze Serikali kwa sababu kuna uwekezaji mkubwa sana
umefanyika katika sekta ya elimu. Kuna mikakati mingi imefanyika
na Serikali ya Awamu ya Sita, lakini nina maswali ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza, pamoja na miradi
hii ya kimkakati kutoa ajira kwa vijana, je, Serikali ina mpango wa
kuweka Sera au miongozo itakayolazimisha miradi yote ya uwekezaji kutenga asilimia maalumu ya ajira za kitaalamu kwa
wahitimu hawa wa vyuo? (Makofi)

Name

Rahma Riyadh Kisuo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, AJIRA NA
MAHUSIANO (MHE. RAHMA R. KISUO): Mheshimiwa Mwenyekiti,
ninakubaliana na mwuliza swali 100% kuwa miradi ya kimkakati
imeonesha uwezo mkubwa wa kuzalisha ajira. Hata hivyo, Sera za
Ajira zinaelekeza ajira zitolewe kwa ushindani bila kutoa
upendeleo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, aidha, Serikali kupitia Ofisi ya Waziri
Mkuu, Wizara ya Kazi, Ajira, na Mahusiano inaendelea kusimamia
utekelezaji wa Sheria ya Kuratibu Ajira za Wageni (Na.1) ya
Mwaka 2015, ambapo pamoja na mambo mengine inaelekeza
wafanyakazi wa kigeni yaani wataalamu kurithisha ujuzi kwa
wazawa katika ajira za kitaalamu ili pale kibali cha kazi cha
wageni kitakapokwisha, mzawa aweze kuchukua nafasi husika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile, Serikali itaendelea kutoa
kipaumbele kwa wafanyakazi wazawa katika miradi ya kimkakati
kwa nafasi za kazi ambazo utaalamu wake siyo adimu katika soko
la ndani ya ajira. (Makofi)

Name

Asha Juma Feruz

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. REGINA C. MALIMA aliuliza:- Je, Serikali imejipangaje kuongeza ajira kwa wahitimu wa vyuo kupitia miradi ya kimkakati, viwanda vidogo, vya kati na programu za ubunifu?

Supplementary Question 2

MHE. ASHA J. FERUZ: Mheshimiwa Mwenyekiti, jina langu ni
Asha Juma Feruz, Mwakilishi ninayewakilisha kundi la Vyuo Vikuu.
Ninaomba kuuliza swali la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, je, Serikali ina mkakati gani
maalumu katika kutumia fursa za ajira katika kundi la vyuo na
vyuo vikuu kupitia mahusiano ya kikanda na kidiplomasia
tuliyonayo hasa zile kozi tunazoziita rare professionals? (Makofi)

Name

Rahma Riyadh Kisuo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, AJIRA NA
MAHUSIANO (MHE. RAHMA R. KISUO): Mheshimiwa Mwenyekiti,
Serikali kwa kushirikiana na vyuo na vyuo vikuu, imeanzisha
mafunzo kwa vitendo kwa wanafunzi wanaoendelea na masomo
katika ngazi mbalimbali za elimu za vyuo na vyuo vikuu na vyuo
vya kati ikiwa ni sehemu ya mtaala ili kuwawezesha kuhitimu elimu
katika ngazi hizo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile, Serikali inatoa Mafunzo ya
Internship yanayojumuisha wahitimu wa ujuzi wa ngazi mbalimbali
za elimu hususan elimu ya juu na kati ambapo wanapatiwa fursa
ya kujifunza kwa vitendo mahali pa kazi. Lengo la mafunzo hayo
ni kuwapatia wahitimu ujuzi, maadili ya kazi, uzoefu na kufanya
kazi za taaluma zao na kuwawezesha kuajirika. (Makofi)